Majogoo wa Anfield Liverpool wakiwa ugenini katika dimba la 'Stadium of light' wameibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Sunderland.
Mshambuliaji Christian Benteke ndiye aliyefunga bao hilo pekee lililoipa timu yake ushindi na pointi tatu muhimu.
Kwa ushindi huo klabu ya Liverpool imejikita katika nafasi ya 7 wakiwa na alama 30 baada ya kucheza michezo 19 msimu huu.
Sunderland maarufu kama Paka Weusi wanasalia katika nafasi ya 19 wakiwa na alama 12 baada ya kucheza michezo 19.