Quantcast
Channel: MPENJA SPORTS
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1447

ARSENAL YAZIDI KUJIIMARISHA KILELENI, MAN U NAO WAFUFUKA

$
0
0
Wayne Rooney amefungia Man Utd bao la ushindi

Arsenal wamefungua mwanya wa alama mbili kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuandikisha ushindi dhidi ya Newcastle, Manchester United nao wakipanda kwa ushindi dhidi ya Swansea City.
Arsenal walilaza Newcastle 1-0, bao lao wakifungiwa na Laurent Koscielny kipindi cha pili, na kufikisha alama 42.
Leicester City wanaowafuata Arsenal walipoteza nafasi ya kujiimarisha baada ya kutoka sare ya 0-0 dhidi ya Bournemouth, licha ya Bournemouth kucheza mwishoni mwa mechi na wachezaji 10 baada ya Simon Francis kuonyeshwa kadi nyekundu kwa kumchezea visivyo mshambuliaji Jamie Vardy.
Riyad Mahrez alishindwa kuwafungia penalti
Uwanjani Old Trafford, ni shangwe kwa meneja Louis van Gaal baada ya vijana wake kuandikisha ushindi wa 2-1, mabao yao mawili wakifungiwa na Anthony Martial na nahodha Wayne Rooney.
Arsenal wamo alama mbili mbele ya Leicester

Kwingineko, Southampton walilazwa 1-0 ugenini Norwich City, bao hilo likifungwa baada ya kiungo wa kati wa Southampton kutoka Kenya Victor Wanyama kupewa kadi nyekundu.
Uwanjani Stadium of Light, Sunderland wamelaza Aston Villa 3-1.
Katika mechi ya awali, Liverpool walilazwa 2-0 na West Ham.
Matokeo kamili:
West Ham 2-0 Liverpool
Arsenal 1 -0 Newcastle
Leicester 0-0 Bournemouth
Man Utd 2-1 Swansea
Norwich 1 -0 Southampton
Sunderland 3-1 Aston Villa
West Brom 2-1 Stoke

Viewing all articles
Browse latest Browse all 1447

Trending Articles