Quantcast
Channel: MPENJA SPORTS
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1447

IBRAHIMOVIC ASEMA HAYA BAADA YA KUSIKIA DI MARIA YUPO KATIKA HATUA ZA MWISHO KUTUA PSG

$
0
0
Zlatan Ibrahimovic amemkaribisha Angel Di Maria Paris Saint-Germain, baada ya taarifa kuwa, uhamisho wa Muargentina huyo ukiwa karibu kabisa kukamilika.
Kocha wa Man United Louis van Gaal jana alitanabaisha  kuwa Di Maria hakuungana na wenzake kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya kama ambavyo ilitarajiwa. 
Kocha wa PSG Laurent Blanc kwa kifupi sana alisema, "uwezekano mkubwa" kwa mchezaji huyo wa zamani wa Real Madrid kujiunga na wababe hao wenye maskani yao Parc des Princes wakati huu wa majira ya joto, na sasa Ibrahimovic amechukua fursa hiyo kumkaribisha nyota huyo.
"Anakaribishwa sana, ataleta vitu vipya hapa, ni mchezaji mzuri", Msweden huyo alikaririwa na Le Parisien. "Ujio wake utaongeza chachu katika timu".


Viewing all articles
Browse latest Browse all 1447

Trending Articles