Quantcast
Channel: MPENJA SPORTS
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1447

NEYMAR NAYE AINGIA KWENYE MTEGO WA UKWEPAJI KODI UHISPANIA

$
0
0
Nyota wa Barcelona Neymar, anashutumiwa kwa kuficha baadhi ya taarifa za mapato yake kuanzia alipokuwa Santos, Barcelona (mpaka sasa) na mikataba yake ya Nike. Mapato hayo yanakadiriwa kufika kiasi cha Yuro milioni 45.9. Vielelezo vya mahakama vinaonyesha kwamba Neymar alitumia makampuni yake (Neymar Sport e Marketing, N & N Consultoria, N & N Administracao de Bens) kukwepa kulipa Yuro mil 56.4 kati ya mwaka 2012 na mwaka 2014.
Jaji alitoa shutuma hizo na kusema kuwa Neymar alikuwa na mikataba feki ili kuficha vyanzo vyake vingine vya mapato. "Tuliangalia kwa makini taarifa kuhusu masuala ya kodi juu ya Neymar, biashara zake tatu na washirika wake katika biashara (wazazi wake) na tulijiridhisha kukuta udanganyifu katika biashara hizo", aliandika Develly Claudia Montez ambaye alikuwa mkaguzi wa mahakama.
Kwa sasa Neymar yuko kwenye shihikizo kubwa la uchunguzi wa tuhuma za ukwepaji kodi dhidi ya serikali ya Uhispania. Huyu si mchezaji wa kwanza wa Barcelona kukumbana na tuhuma kama hizi, kwani nyota mwingine wa klabu hiyo Lionel Messi na Javier Mascherano pia waliingia katika mtego huo.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 1447

Trending Articles